KWA NINI UKATE TAMAA NA REHMA ZA ALLAH SUBHAANAHUU WATAALA?
Katika makala iliyopita tuliona baadhi ya Mitume wa Allah walioteleza
kibinadamu na Wakatambua kosa wakarudi kwa Allah na Allah akawasamehe.
Allah subhaanahu wataala anasema katika Suratul-Qasas:{15-16} akielezea namna Nabii Mussa Alayhi salaam alipowakuta watu wawili wakipigana “. Na aliingia mjini wakati wenyeji wake walikuwa katika ghafla, na akakuta humo watu wawili wakipigana: huyu wa jamii yake na huyu wa adui zake. Ndipo Musa akampiga ngumi, na akammaliza.
Akasema: Hili ni tendo la Shetani; bila shaka yeye ni adui, mpotezaji dhahiri. Akasema: Mola wangu! Bila shaka nimedhulumu nafsi yangu, basi Unisamehe; naye Akamsamehe. Kwa yakini Yeye ni Msamehevu,Mrehemevu”
Allah akamsamehe dhambi yake ile yakuuwa.
Mwangalie Nabii Ayuub Alayhi salaam alipopewa kazi ya kulingania na kutoifanya akakimbia na kupanda jahazi ikatokea gharka na kutoswa baharini na kumezwa na chewa, akajua kuwa alikosea akamrudia mola wake na Allah anasema katika Qur-an “Na pale ayuub aliponadi na kuomba katika tumbo la chewa “LAAILAAHA ILLA ANTA SUBHAANAK INNIY KUNTU MINADHWAALIMIIN”
“Hakuna Mola apasae kuabudiwa ila wewe, Umeatakasika hakika mimi nilikua miongoni wa waliozidhulumu nafsi zao”
Allah akamsamehe na akamuamrisha chewa amtapike katika ufukwe wa bahari na akamuotesha mti achukue majani yake na kufanya dawa.
JE MIMI NA WEWE HATUJAMKOSEA MOLA WETU?!!!!!!!
Mtume Muhammad (Swalla Allahu alayhi wasallam) amezungumza katika hadithi nyingi kuhusiana na kuomba toba na msamaha kwa Allah subhaanahuu wataala.
Kutoka kwa Abii Hurayra Radhi za Allah ziwe juu yake amesema, nimemsikia Mtume (Swalla Allahu alayhi wasallam) akisema: Naapa kwa jina la Allah, hakika yangu namuomba msamaha na kutubia kwake zaidi ya mara sabiini” {Bukhary}
Akasema tena Mtume (Swalla Allahu alayhi wasallam) katika hadithi aliyoipokea Abii Mussa Al-Ash’ariy “Hakika ya Allah anafungua rehma zake usiku kwa kuwasamehe waliomkosea mchana, na anafungua rehma zake mchana kwa kuwasamehe waliomkosea usiku mpaka jua litakapozama” {Muslim}
kutoka kwa Abii Abdul Rahmaan Abdallah bin Umar bin Khatwaab radhi za Allah ziwe juu yao kutoka kwa Mtume (Swalla Allahu alayhi wasallam) amesema ” Hakika ya Allah anakubali toba ya mja wakati hajafikwa na mauti” {Attirmidhiy}
Sasa ndugu yangu muislamu unadhambi wingi gani kushinda msamaha na rehma za Allah Subhaanahuu wataala?
Msikilize Allah anakwambiaje?
“Sema, Enyi waja wangu mliodhulumu nafsi zenu, Msikate tamaa na rehma ya Mwenyezi Mungu; bila shaka Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote; hakika yeye ni mwingi wa kurehemu”
” (Hao ndio) wanaotubu, wanaoabudu, wanaotukuza, wanaofunga
saumu, wanaorukuu, wanaosujudu, wanaoamuru yaliyo mema, na
wanaozuia yaliyo mabaya, na wanaohifadhi mipaka ya Mwenyezi
Mungu – na wape habari njema waaminio” {9:111}
Kaa chini tubu dhambi zako kwa toba ya kweli na kudhamiria kutorejea tena na kujuta kwa yale uliyoyafanya na Allah ni mwema atasikia kilio chako na atakusamehe usikate tamaa na rehma za Allah.
Allah subhaanahu wataala anasema katika Suratul-Qasas:{15-16} akielezea namna Nabii Mussa Alayhi salaam alipowakuta watu wawili wakipigana “. Na aliingia mjini wakati wenyeji wake walikuwa katika ghafla, na akakuta humo watu wawili wakipigana: huyu wa jamii yake na huyu wa adui zake. Ndipo Musa akampiga ngumi, na akammaliza.
Akasema: Hili ni tendo la Shetani; bila shaka yeye ni adui, mpotezaji dhahiri. Akasema: Mola wangu! Bila shaka nimedhulumu nafsi yangu, basi Unisamehe; naye Akamsamehe. Kwa yakini Yeye ni Msamehevu,Mrehemevu”
Allah akamsamehe dhambi yake ile yakuuwa.
Mwangalie Nabii Ayuub Alayhi salaam alipopewa kazi ya kulingania na kutoifanya akakimbia na kupanda jahazi ikatokea gharka na kutoswa baharini na kumezwa na chewa, akajua kuwa alikosea akamrudia mola wake na Allah anasema katika Qur-an “Na pale ayuub aliponadi na kuomba katika tumbo la chewa “LAAILAAHA ILLA ANTA SUBHAANAK INNIY KUNTU MINADHWAALIMIIN”
“Hakuna Mola apasae kuabudiwa ila wewe, Umeatakasika hakika mimi nilikua miongoni wa waliozidhulumu nafsi zao”
Allah akamsamehe na akamuamrisha chewa amtapike katika ufukwe wa bahari na akamuotesha mti achukue majani yake na kufanya dawa.
JE MIMI NA WEWE HATUJAMKOSEA MOLA WETU?!!!!!!!
Mtume Muhammad (Swalla Allahu alayhi wasallam) amezungumza katika hadithi nyingi kuhusiana na kuomba toba na msamaha kwa Allah subhaanahuu wataala.
Kutoka kwa Abii Hurayra Radhi za Allah ziwe juu yake amesema, nimemsikia Mtume (Swalla Allahu alayhi wasallam) akisema: Naapa kwa jina la Allah, hakika yangu namuomba msamaha na kutubia kwake zaidi ya mara sabiini” {Bukhary}
Akasema tena Mtume (Swalla Allahu alayhi wasallam) katika hadithi aliyoipokea Abii Mussa Al-Ash’ariy “Hakika ya Allah anafungua rehma zake usiku kwa kuwasamehe waliomkosea mchana, na anafungua rehma zake mchana kwa kuwasamehe waliomkosea usiku mpaka jua litakapozama” {Muslim}
kutoka kwa Abii Abdul Rahmaan Abdallah bin Umar bin Khatwaab radhi za Allah ziwe juu yao kutoka kwa Mtume (Swalla Allahu alayhi wasallam) amesema ” Hakika ya Allah anakubali toba ya mja wakati hajafikwa na mauti” {Attirmidhiy}
Sasa ndugu yangu muislamu unadhambi wingi gani kushinda msamaha na rehma za Allah Subhaanahuu wataala?
Msikilize Allah anakwambiaje?
“Sema, Enyi waja wangu mliodhulumu nafsi zenu, Msikate tamaa na rehma ya Mwenyezi Mungu; bila shaka Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote; hakika yeye ni mwingi wa kurehemu”
” (Hao ndio) wanaotubu, wanaoabudu, wanaotukuza, wanaofunga
saumu, wanaorukuu, wanaosujudu, wanaoamuru yaliyo mema, na
wanaozuia yaliyo mabaya, na wanaohifadhi mipaka ya Mwenyezi
Mungu – na wape habari njema waaminio” {9:111}
Kaa chini tubu dhambi zako kwa toba ya kweli na kudhamiria kutorejea tena na kujuta kwa yale uliyoyafanya na Allah ni mwema atasikia kilio chako na atakusamehe usikate tamaa na rehma za Allah.
HIJABU YA MWANAMKE WA KIISLAM KATIKA QUR-AN NA SUNNA
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma na mwenye kurehemu.
Kila sifa njema na shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu wote. Sala na amani ziwe juu ya ya mja wake na Mtume wake Nabii Muhammad (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) ambae ametumwa kuwa mwalimu na rehma kwa walimwengu wote.
Ni kweli na ni hakika kwamba inasikitisha sana kwa wanawake mbali
mbali wa Kiislam kwa namna ya mavazi wanayovaa kila siku
zinavyokwenda, aiku hizi wanawake wengi wamekuwa wakivaa mavazi yasiyo na stara, wanavaa mavazi ya kikafiri, ambapo ukiwaangalia utaona kuwa hakuna tofauti baina yao na Mayahudi au hata Wakristo, na hali hii imekuwa ni hatari kubwa sana katika maisha ya Uislam, na kupelekea au kusababisha kushuka kwa hasira ya Mwenyezi Mungu na yakateremka maangamizo na kuangamia wema na wabaya.
Na lengo ni wale mawalii amri wa hao wanawake wanawaachia wake zao na mabinti zao na dadfa zao kuvaa nguo za kikafiri na kutoka nje ya nyumba zao bila ya kuvaa baibui na hijaab. Na yakizodi mambo haya ni sababu ya kushuka maangamizo kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote wabaya na wema.
Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Surat Al-Anfaal aya ya 25
amesema:- “NA IOGOPENI ADHABU YA MWENYEZI MUNGU HAPA DUNIANI AMBAYO HAITAWASIBU PWKW YAO WALE WALIODHULUMU NAFSI ZAO MIONGONI MWENU BALI ITAWASIBU HATA WALIONYAMAZA WASIYAKATAZE MAOVU. NA WENGINEO PIA. NA JUENI YA KWAMBA MWENYEZI MUNGU NI MKALI WA KUADHIBU.”
Kutokana na ukali wa aya hiyo ya Mwenyezi Mungu enyi Mawalii amri wakatazeni wake zenu mabinti zenu na dada zenu, na waamrisheni waisitiri miili yao, na iogopeni adhabu ya Mwenyezi Mungu, la si hivyo mtasababisha kuwashukia hasira ya Mwenyezi Mungu kwa wote.
Uislam ni Dini iliyoleta sheria na adabu za Kiislam, na baadhi yake ni
sheria ya vazi la Kiislam kwa wanawake wa Kiislam.
Wanawake wa kiislam wamekuwa na tabia mbaya iliyo kinyume na
maamrisho ya dini yao kwa kwenda makazini kukaa mabarazani au
hata kupita katika masoko wakiwa uchi, wanaonesha miili yao ovyo
kwa wanaume wanaoweza kuwaoa (Ajnabi) bila hata kuwa na hofu
juu ya Mola wao au hata kuona haya ama aibu ya aina yeyete ile.
Na tabia hii ni katika mambo mabaya sana na ni hatari kubwa sana
katika jamii ya Kiislam kwa haya maasi makubwa kabisa
yanayofanywa na wanawake ikiwa ni dada zetu mama zetu wake
zetu au hata mabinti zetu na hata wa wenzetu.
Hijaab ya mwanamke wa Kiislam imekuja kwa malengo maalum kama sheria ya kustiri miili ya wanawake, kwa kuamrishwa wanawake wa Kiislam kuisitiri miili yao kwani kufanya hivyo ni salama kwao na ni kuepukana na Shetani kwa kufanya mambo machafu na mengine yaliyokuwa mabaya na yenye kuvutia matamanio mabaya.
Sharia ni lazima kwa kila walii, ambao ni wazazi, au waume au kaka
au ndugu, na wanatakiwa wasinyamaze na kuwaregezea watu wao wa kike kutoka katika misingi ya sheria na adabu ya Kiislam.
Tabia hii ya kuwaachia wanawake inawapasa (wanaume) au hata
wanawake kuikataza jamii nzima ya wanawake wa Kiislam na
wasiachiwe kabisa kuvaa mavazi ya kikafiri na kutoka nayo nje bila
ya kusitiri miili yao.
Faradhi hii ni ya kila Muislam ya kuamrisha mema na kukataza
mabaya, kwani kunyamaza kimya bila ya kukataza mabaya ni sababu kubwa ya kutyokea maafa mbali mbali katika jamii ya Waislam na hatimae kufikwa na maangamizo.
Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:-
“HAKIKA WATU WANAPOONA MABAYA YANAFANYIKA KISHA
WASIYABADILI KWA KUYAKATAZA, WAKANYAMAZA NA KUPUUZA BASI IMEKARIBIA KUWASHUKIA ADHABU YA MWENYEZI MUNGU”
Na katika Qur-an Mwenyezi Mungu Mtukufu sehemu nyingi
amesimulia habari za maangamizo waliyoangamizwa watu wa Israil
kutokana na kutokataza mabaya, walikuwa wanaona mabaya
yanafanyika laini walibyamaza kimya bila ya kukatazana, na hapo
ndipo ilipowashukia laana na adhabu ya Mwenyezi Mungu juu yao
kutokana na kunyamaza kimya kwao.
Katika Surat Al-Maaida aya ya 78/79 Mwenyezi Mungu amesema:-
“WALILAANIWA WALE WALIOKUFURU MIONGONI MWA WANA WA ISRAIL KWA ULIMI WA NABII DAUD NA NABII ISSA IBN MARYAM. HAYO NI KWA SABABU WALIASI NA WAKIRUKA MIPAKA YA MWENYEZI MUNGU. HAWAKUWA WENYE KUKATAZANA MAMBO MABAYA WALIYOKUWA WAKIYAFANYA, MAOVU YALIOJE YA MAMBO HAYO MABAYA WALIYOKUWA WAKIYAFANYA.?
Hiyo ndiyo hatari ya kuyaona mabaya yanafanywa kasha watu
wakanyamaza kimya bila hata kuyakataza.
Sasa hao mawalii (wazee ikiwa ni wanaume au hata wanawake) wa
kina dada, wake au mabinti ndio waliolazimika kuyasimamia na
kuwakataza wanawake kuvaa mavazi ya kikafiri sio kuregeza na
kunyamaza kimya.
Lakini utakuta hao mawalii wenyewe wamenyamaza, na kunyamaza
kwao ina maanishwa kuwa wako radhi kuwaachia watoto wao, wake
zao, dada zao au hata mama zao kuonesha miili yao kwa watu ajnabi.
Na hii ndio sababu ya kushuka hasira na adhabu za Mwenyezi Mungu wakaangamia wema na wabaya kutokana kunyamaza kwa
kutoyakataza mabaya.
Basi hapo laana ya Mwenyezi Mungu humpata kila mtu. Na ni sababu za maangamizo zinakuwa namana hiyo za kutokataza mabaya na kunyamaza kimya.
Na hao mawalii wananyamaza na kuwaachia wake zao na dada zao na watoto wao kuvaa nguo za kubana na kutoka nje bila ya kuvaa hata baibui, wanaonesha miili yao ovyo huko nje. Kila mtru ajnabi huko nje anausoma mwili wa mwanamke ulivyo, na hali huyo mwanamke ni Muislam.
Tujiulize je huyo tutamwita kuwa ni mwanamke wa Kiislam? Kichwa
chake kiwazi na ikiwa kajitanda basi huo mtandio si wa sitara, bali
mtandio wa pambo tu, kichwa chote kinaonekana. Au atafunika
kichwa vizuri kwa huo mtandio au ushungi lakini, lakini kava nguo za
kubana, mwili wake wote unaonekana, unamuona viumgo vyote vya
mwili wake, jee! Huyo tuamwita mwanamke wa Kiislam?
Mwanamke wa namna hiyo yeye na kafiri ni sawa kabisa, hana
Uislam wowote, na hali ya kuwa Uislam umeleta sheria ya vazi la
wanawake wastiri miili yao.
Mwenyezi Mungu Mtukufu alipokuwa akiwahutubia wake wa Mtume
Muhammad (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam) ambapo
hotuba inayowahusu wake wa mtume ni kwa ajili ya Waislam wote.
Amesema katika Surat Al Ahzab aya ya 33:-“NA KAENI MAJUMBANI MWENU WALA MSIONESHE MAPAMBO YA MIILI YENU KAMA WALIVYOKUWA WAKIONESHA MAPAMBO YAO WANAWAKE WA ZAMA ZA UJAHILIYA.?
Wafasiri wa aya hii wamesema maana ya ?TABARRUJIL-
JAAHILIYYAH? Ya kuwa ni kuonesha mwanamke namna ya pambo la mwili wake ulivyo ili avutike mwanamme aingiwe na matamanio
mabaya ya zanaa.
Katika zama za ujahiliya mwanamke alikuwa anajitahidi kuupamba
mwili wake na kuvaa nguo za kubana na nyepesi ili mwili wake
uonekane vizuri na wanaume, basi mwanamme yeyote tule akimuona
tu mwanamke alievaa nguo za kubana namna hiyo akauona mwili wa mwanamke huyo, hupiga katika moyo wake tamanio baya
unamsadikisha na kuingia katika maovu ya kuzini. Hivi ndivyo
walivyotafsiri wataalam juu ya maana ya ?TABARRUJIL-
JAAHILIYYAH? Ni kwamba kuonesha pamno la mwili wake mwanamke ili avutike mwanamme kwa tamanio la zinaa.
Vile vile maana ya ?TABARRUJIL-JAAHILIYYAH? imetafsiriwa kuwa
ni kuonesha mwili wake mwanamke na kutembe utembezji wa kudeka na kulainika mwili wake na kuilegeza miguu yake katika mwendo wake wa kuilegeza shingo yake ili kichwa chake kilegee kwa kunyongeka na kulainika kama ilivyolainika nundu ya ngamia, maana wale ngami walionona wakitembea nundu zao hulainika na hunama mara kulia na mara kushoto.
Basi wanawake waliotajwa kuhusu ?TABARRUJIL-JAAHILIYYAH?
ndio vichwa vyao sawa na hizo nundu za ngamia, na kuvaa nguo
ambazo si za stara. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:-“WANAWAKE WAMEVAA MAVAZI YA UCHI (YAANI NGUO SI ZA STARA) WAMEELEMEA KUINAMA (KUPENDA MAVAZI YASIYOKUWA YA STARA), VICHWA VYAO KAMA NUNDU ZA NGAMIA VIMEINAMA HAWATAINGIA PEPONI WALA HAWATAPATA (HATA) HARUFU YAKE (PEPO).?
Ndio nguo wanazovaa wanawake siku hizi za kukaa uchi tu, si nguo za stara, bali nguo za mapambo ya kuonesha miili yao, ambazo
alizozitaja Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam).
Na Mwenyezi Mungu kabainisha namna ya nguo za Kiislam na sheria kwa mwanamke wa Kiislam amelazimisghwa avae kwa ajili ya kusitiri mwili wake.
Mungu atupe kila la kheri na mafanikio amiiin.
Kila sifa njema na shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu wote. Sala na amani ziwe juu ya ya mja wake na Mtume wake Nabii Muhammad (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) ambae ametumwa kuwa mwalimu na rehma kwa walimwengu wote.
Ni kweli na ni hakika kwamba inasikitisha sana kwa wanawake mbali
mbali wa Kiislam kwa namna ya mavazi wanayovaa kila siku
zinavyokwenda, aiku hizi wanawake wengi wamekuwa wakivaa mavazi yasiyo na stara, wanavaa mavazi ya kikafiri, ambapo ukiwaangalia utaona kuwa hakuna tofauti baina yao na Mayahudi au hata Wakristo, na hali hii imekuwa ni hatari kubwa sana katika maisha ya Uislam, na kupelekea au kusababisha kushuka kwa hasira ya Mwenyezi Mungu na yakateremka maangamizo na kuangamia wema na wabaya.
Na lengo ni wale mawalii amri wa hao wanawake wanawaachia wake zao na mabinti zao na dadfa zao kuvaa nguo za kikafiri na kutoka nje ya nyumba zao bila ya kuvaa baibui na hijaab. Na yakizodi mambo haya ni sababu ya kushuka maangamizo kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote wabaya na wema.
Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Surat Al-Anfaal aya ya 25
amesema:- “NA IOGOPENI ADHABU YA MWENYEZI MUNGU HAPA DUNIANI AMBAYO HAITAWASIBU PWKW YAO WALE WALIODHULUMU NAFSI ZAO MIONGONI MWENU BALI ITAWASIBU HATA WALIONYAMAZA WASIYAKATAZE MAOVU. NA WENGINEO PIA. NA JUENI YA KWAMBA MWENYEZI MUNGU NI MKALI WA KUADHIBU.”
Kutokana na ukali wa aya hiyo ya Mwenyezi Mungu enyi Mawalii amri wakatazeni wake zenu mabinti zenu na dada zenu, na waamrisheni waisitiri miili yao, na iogopeni adhabu ya Mwenyezi Mungu, la si hivyo mtasababisha kuwashukia hasira ya Mwenyezi Mungu kwa wote.
Uislam ni Dini iliyoleta sheria na adabu za Kiislam, na baadhi yake ni
sheria ya vazi la Kiislam kwa wanawake wa Kiislam.
Wanawake wa kiislam wamekuwa na tabia mbaya iliyo kinyume na
maamrisho ya dini yao kwa kwenda makazini kukaa mabarazani au
hata kupita katika masoko wakiwa uchi, wanaonesha miili yao ovyo
kwa wanaume wanaoweza kuwaoa (Ajnabi) bila hata kuwa na hofu
juu ya Mola wao au hata kuona haya ama aibu ya aina yeyete ile.
Na tabia hii ni katika mambo mabaya sana na ni hatari kubwa sana
katika jamii ya Kiislam kwa haya maasi makubwa kabisa
yanayofanywa na wanawake ikiwa ni dada zetu mama zetu wake
zetu au hata mabinti zetu na hata wa wenzetu.
Hijaab ya mwanamke wa Kiislam imekuja kwa malengo maalum kama sheria ya kustiri miili ya wanawake, kwa kuamrishwa wanawake wa Kiislam kuisitiri miili yao kwani kufanya hivyo ni salama kwao na ni kuepukana na Shetani kwa kufanya mambo machafu na mengine yaliyokuwa mabaya na yenye kuvutia matamanio mabaya.
Sharia ni lazima kwa kila walii, ambao ni wazazi, au waume au kaka
au ndugu, na wanatakiwa wasinyamaze na kuwaregezea watu wao wa kike kutoka katika misingi ya sheria na adabu ya Kiislam.
Tabia hii ya kuwaachia wanawake inawapasa (wanaume) au hata
wanawake kuikataza jamii nzima ya wanawake wa Kiislam na
wasiachiwe kabisa kuvaa mavazi ya kikafiri na kutoka nayo nje bila
ya kusitiri miili yao.
Faradhi hii ni ya kila Muislam ya kuamrisha mema na kukataza
mabaya, kwani kunyamaza kimya bila ya kukataza mabaya ni sababu kubwa ya kutyokea maafa mbali mbali katika jamii ya Waislam na hatimae kufikwa na maangamizo.
Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:-
“HAKIKA WATU WANAPOONA MABAYA YANAFANYIKA KISHA
WASIYABADILI KWA KUYAKATAZA, WAKANYAMAZA NA KUPUUZA BASI IMEKARIBIA KUWASHUKIA ADHABU YA MWENYEZI MUNGU”
Na katika Qur-an Mwenyezi Mungu Mtukufu sehemu nyingi
amesimulia habari za maangamizo waliyoangamizwa watu wa Israil
kutokana na kutokataza mabaya, walikuwa wanaona mabaya
yanafanyika laini walibyamaza kimya bila ya kukatazana, na hapo
ndipo ilipowashukia laana na adhabu ya Mwenyezi Mungu juu yao
kutokana na kunyamaza kimya kwao.
Katika Surat Al-Maaida aya ya 78/79 Mwenyezi Mungu amesema:-
“WALILAANIWA WALE WALIOKUFURU MIONGONI MWA WANA WA ISRAIL KWA ULIMI WA NABII DAUD NA NABII ISSA IBN MARYAM. HAYO NI KWA SABABU WALIASI NA WAKIRUKA MIPAKA YA MWENYEZI MUNGU. HAWAKUWA WENYE KUKATAZANA MAMBO MABAYA WALIYOKUWA WAKIYAFANYA, MAOVU YALIOJE YA MAMBO HAYO MABAYA WALIYOKUWA WAKIYAFANYA.?
Hiyo ndiyo hatari ya kuyaona mabaya yanafanywa kasha watu
wakanyamaza kimya bila hata kuyakataza.
Sasa hao mawalii (wazee ikiwa ni wanaume au hata wanawake) wa
kina dada, wake au mabinti ndio waliolazimika kuyasimamia na
kuwakataza wanawake kuvaa mavazi ya kikafiri sio kuregeza na
kunyamaza kimya.
Lakini utakuta hao mawalii wenyewe wamenyamaza, na kunyamaza
kwao ina maanishwa kuwa wako radhi kuwaachia watoto wao, wake
zao, dada zao au hata mama zao kuonesha miili yao kwa watu ajnabi.
Na hii ndio sababu ya kushuka hasira na adhabu za Mwenyezi Mungu wakaangamia wema na wabaya kutokana kunyamaza kwa
kutoyakataza mabaya.
Basi hapo laana ya Mwenyezi Mungu humpata kila mtu. Na ni sababu za maangamizo zinakuwa namana hiyo za kutokataza mabaya na kunyamaza kimya.
Na hao mawalii wananyamaza na kuwaachia wake zao na dada zao na watoto wao kuvaa nguo za kubana na kutoka nje bila ya kuvaa hata baibui, wanaonesha miili yao ovyo huko nje. Kila mtru ajnabi huko nje anausoma mwili wa mwanamke ulivyo, na hali huyo mwanamke ni Muislam.
Tujiulize je huyo tutamwita kuwa ni mwanamke wa Kiislam? Kichwa
chake kiwazi na ikiwa kajitanda basi huo mtandio si wa sitara, bali
mtandio wa pambo tu, kichwa chote kinaonekana. Au atafunika
kichwa vizuri kwa huo mtandio au ushungi lakini, lakini kava nguo za
kubana, mwili wake wote unaonekana, unamuona viumgo vyote vya
mwili wake, jee! Huyo tuamwita mwanamke wa Kiislam?
Mwanamke wa namna hiyo yeye na kafiri ni sawa kabisa, hana
Uislam wowote, na hali ya kuwa Uislam umeleta sheria ya vazi la
wanawake wastiri miili yao.
Mwenyezi Mungu Mtukufu alipokuwa akiwahutubia wake wa Mtume
Muhammad (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam) ambapo
hotuba inayowahusu wake wa mtume ni kwa ajili ya Waislam wote.
Amesema katika Surat Al Ahzab aya ya 33:-“NA KAENI MAJUMBANI MWENU WALA MSIONESHE MAPAMBO YA MIILI YENU KAMA WALIVYOKUWA WAKIONESHA MAPAMBO YAO WANAWAKE WA ZAMA ZA UJAHILIYA.?
Wafasiri wa aya hii wamesema maana ya ?TABARRUJIL-
JAAHILIYYAH? Ya kuwa ni kuonesha mwanamke namna ya pambo la mwili wake ulivyo ili avutike mwanamme aingiwe na matamanio
mabaya ya zanaa.
Katika zama za ujahiliya mwanamke alikuwa anajitahidi kuupamba
mwili wake na kuvaa nguo za kubana na nyepesi ili mwili wake
uonekane vizuri na wanaume, basi mwanamme yeyote tule akimuona
tu mwanamke alievaa nguo za kubana namna hiyo akauona mwili wa mwanamke huyo, hupiga katika moyo wake tamanio baya
unamsadikisha na kuingia katika maovu ya kuzini. Hivi ndivyo
walivyotafsiri wataalam juu ya maana ya ?TABARRUJIL-
JAAHILIYYAH? Ni kwamba kuonesha pamno la mwili wake mwanamke ili avutike mwanamme kwa tamanio la zinaa.
Vile vile maana ya ?TABARRUJIL-JAAHILIYYAH? imetafsiriwa kuwa
ni kuonesha mwili wake mwanamke na kutembe utembezji wa kudeka na kulainika mwili wake na kuilegeza miguu yake katika mwendo wake wa kuilegeza shingo yake ili kichwa chake kilegee kwa kunyongeka na kulainika kama ilivyolainika nundu ya ngamia, maana wale ngami walionona wakitembea nundu zao hulainika na hunama mara kulia na mara kushoto.
Basi wanawake waliotajwa kuhusu ?TABARRUJIL-JAAHILIYYAH?
ndio vichwa vyao sawa na hizo nundu za ngamia, na kuvaa nguo
ambazo si za stara. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:-“WANAWAKE WAMEVAA MAVAZI YA UCHI (YAANI NGUO SI ZA STARA) WAMEELEMEA KUINAMA (KUPENDA MAVAZI YASIYOKUWA YA STARA), VICHWA VYAO KAMA NUNDU ZA NGAMIA VIMEINAMA HAWATAINGIA PEPONI WALA HAWATAPATA (HATA) HARUFU YAKE (PEPO).?
Ndio nguo wanazovaa wanawake siku hizi za kukaa uchi tu, si nguo za stara, bali nguo za mapambo ya kuonesha miili yao, ambazo
alizozitaja Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa aalihi wa sallam).
Na Mwenyezi Mungu kabainisha namna ya nguo za Kiislam na sheria kwa mwanamke wa Kiislam amelazimisghwa avae kwa ajili ya kusitiri mwili wake.
Mungu atupe kila la kheri na mafanikio amiiin.