Prophet Muhammad (saw) was the final Messenger of Allah to humanity, and the Noble Qur'an is the last Message was sent to us. Its predecessors such as the Torah, Psalms, and Gospels have all been superseded.The Qur'an of today is the same as the Qur'an revealed to Muhammad (saw) 1400 years ago.
Weather
Tuesday, February 3, 2015
KAMA HUSIMAMISHI SWALA NA PEPO HUTOIONA
Tumesahau ya kwamba wenye kutupwa motoni wanatokana na
kuacha kusimamisha Swalah? Qur-aan Tukufu yatueleza (tafsiri):
{{"Ni kipi kilichokupelekeni Motoni?" Waseme: "Hatukuwa miongoni
mwa waliokuwa wakiswali…"}} [al-Muddaththir: 42-43]
Hadiyth ifuatayo inafafanua zaidi (tafsiri):
Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘Anhu): hakika amesema
Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa
sallam): ((Umma wangu wote utaingia Peponi isipokuwa kwa
atakayekataa)) Pakasemwa: na ni nani huyo atakayekataa ewe
Mjumbe wa Allaah? Akasema: ((Mwenye kunitii mimi ataingia Peponi,
na atakayeniasi basi huyo amekataa)). [Imepokelewa na Al-Bukhaariy,
Buluughul-Maraami, Hadiyth ya 157]
Ila yahitajika juhudi na kuonesha moyo wa kumukhofu Allaah
(Subhaanahu wa Ta’ala). Tusitegemee tulale tuu halafu tushushiwe
riziki kama alivyofanyiwa bibi Maryam '(Radhiya Allaahu ‘Anha).
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment